Twenzetu Duniani Na SportPesa 100Mil - Vigezo Na Masharti
Muhtasari wa Promosheni
SportPesa Tanzania inafurahia kutambulisha Promosheni ya Twenzetu Duniani na SportPesa, itakayofanyika katika kipindi cha Kombe la Dunia 2026. Promosheni hii inawapa wateja wanaostahili fursa mbalimbali za kushinda zawadi za fedha kila wiki pamoja na kufuzu kushiriki Droo Kuu kwa kuweka beti zinazokidhi vigezo kupitia majukwaa ya SportPesa katika kipindi cha promosheni. Kushiriki katika promosheni hii kunamaanisha kukubali Masharti na Vigezo hivi.
Beti yoyote inayokidhi vigezo iliyowekwa kuanzia tarehe 16 Juni 2026 hadi 19 Julai 2026 saa 23:59 kwa saa za Afrika Mashariki (EAT) itastahili kushiriki katika promosheni hii. Wateja wataingizwa moja kwa moja kwenye promosheni kwa kuweka beti zinazokidhi vigezo katika kipindi cha promosheni. Hakuna usajili wa ziada unaohitajika. Kila beti inayokidhi vigezo itampa mteja nafasi moja ya kushiriki kwenye droo husika.
SUKA MKEKA WAKO HAPA AU CHEZA KASINO
Ustahiki wa Kushiriki
Promosheni hii iko wazi kwa:
a. Wateja waliosajiliwa wa SportPesa Tanzania.
b. Wateja wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
c. Wateja wanaoweka beti zinazokidhi vigezo katika kipindi cha promosheni.
Wafuatao hawastahili kushiriki:
- Watu wenye umri chini ya miaka 18.
- Wafanyakazi wa SportPesa Tanzania na kampuni zake washirika.
- Wanafamilia wa karibu wa wafanyakazi wa SportPesa.
- Mtu yeyote anayekatazwa kisheria kushiriki katika shughuli za ubashiri au michezo ya kubahatisha.
Beti Zinazokidhi Vigezo
1. Aina zifuatazo za beti zinastahili kushiriki katika promosheni:
- Single Bets
- Multi Bets
- Live Bets
- Jackpot Products
- Mid-week Jackpot
- Supa Jackpot
- Michezo yote ya Casino inayopatikana SportPesa Tanzania katika kipindi cha promosheni..
- Beti zilizofutwa (Cancelled) au zilizobatilishwa (Voided) hazitastahili kushiriki kwenye promosheni.
- Hakuna kiwango cha juu cha idadi ya nafasi ambazo mteja anaweza kupata kupitia beti zinazokidhi vigezo.
Droo za Kila Wiki
Katika kipindi chote cha promosheni, SportPesa itaendesha droo za kila wiki
- Jumla ya washindi 100 watachaguliwa kila wiki.
- Washindi wa kila wiki watapokea fedha kwenye pochi zao za mchezo (wallet) kulingana na maamuzi ya SportPesa Tanzania.
- Tarehe za droo za kila wiki pamoja na mgawanyo wa zawadi zitatangazwa kupitia njia rasmi za mawasiliano za SportPesa.
- Wateja watakaoshinda zawadi za kila wiki wataendelea kustahili kushiriki katika Droo Kuu. Hivyo, mteja anaweza kushinda zaidi ya zawadi moja katika kipindi cha promosheni.
Droo Kuu ya Fainale
Droo Kuu ya Fainale itafanyika tarehe 20 Julai 2026.
- Wateja wote wenye beti zinazokidhi vigezo zilizokusanywa katika kipindi chote cha promosheni watastahili kushiriki katika Droo Kuu.
- Jumla ya washindi 10 watachaguliwa kutoka kwenye nafasi zote zilizokusanywa katika kipindi cha promosheni.
- Zawadi ya Droo Kuu itagawanywa kwa usawa kati ya washindi 10.
- Washindi watajulishwa na SportPesa Tanzania kabla ya hafla ya utoaji wa zawadi ili kusaidia maandalizi ya usafiri kwa washindi watakaotoka mikoani.
Uchaguzi wa Washindi
- Washindi watachaguliwa kupitia mfumo wa kompyuta wa droo za bahati nasibu utakaosimamiwa na SportPesa Tanzania.
- SportPesa ina haki ya kuteua wakaguzi huru, wadhibiti au wawakilishi wa upande wa tatu kusimamia mchakato wa droo pale itakapohitajika.
- Matokeo yote ya droo yatakuwa ya mwisho.
Kuwataarifu Washindi
- Washindi wa kila wiki watajulishwa kupitia SMS na arifa za Push zitakazotumwa kwenye namba iliyosajiliwa kwenye akaunti yao ya SportPesa.
- Washindi wa Droo Kuu watawasiliana kupitia simu kutoka Kitengo cha Huduma kwa Wateja kwa kutumia namba iliyosajiliwa kwenye akaunti yao ya SportPesa.
- Endapo mshindi wa Droo Kuu hatapatikana baada ya jitihada za kutosha kufanyika, SportPesa ina haki ya kuchagua mshindi mbadala.
- Wateja wanawajibika kuhakikisha taarifa za akaunti zao ni sahihi na zimeboreshwa wakati wote.
Malipo ya Zawadi Za Promosheni
- Zawadi zote za promosheni zitawekwa au kulipwa kupitia njia itakayoamuliwa na SportPesa Tanzania.
- SportPesa ina haki ya kuthibitisha utambulisho wa mshindi kabla ya malipo ya zawadi kufanyika.
- Kushindwa kutoa nyaraka za uthibitisho zinazokubalika kunaweza kusababisha mshindi kupoteza haki ya kupata zawadi.
Matumizi ya Taarifa za Washindi kwa Madhumuni ya Utangazaji
Kwa kushiriki katika Droo Kuu, washindi wanakubali kuwa SportPesa Tanzania inaweza kutumia jina lao, picha, sauti, video na ushuhuda wao kwa madhumuni ya matangazo, masoko na utangazaji bila malipo yoyote ya ziada.
Kukubali Masharti na Vigezo
- Kushiriki katika Promosheni ya Twenzetu Duniani Na SportPesa kunamaanisha kukubali kikamilifu Masharti na Vigezo hivi.
- Masharti na Vigezo hivi vitasomwa pamoja na Masharti na Vigezo ya Jumla ya SportPesa Tanzania yanayopatikana kwenye tovuti ya kampuni. Kwa masuala ambayo hayajaelezwa moja kwa moja katika Masharti haya, Masharti na Vigezo ya Jumla yatatumika. Endapo kutakuwa na mgongano au kutokuelewana kati ya masharti hayo mawili, Masharti na Vigezo vya Promosheni hii vitatumika kwa promosheni hii pekee.
Uchezaji wa Kuwajibika
- Ubashiri unaruhusiwa kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea pekee.
- SportPesa Tanzania inahamasisha uchezaji wa kuwajibika wakati wote.
- Wateja wanashauriwa kucheza kwa uwajibikaji na kwa kuzingatia uwezo wao wa kifedha.
Ubashiri unapaswa kuwa burudani. Ikiwa unahisi kuwa ubashiri wako unakuwa tatizo, tafadhali tembelea sportpesa.co.tz/responsible-gaming au wasiliana na timu yetu ya Huduma kwa Wateja inayopatikana saa 24 kwa siku, siku 7 za wiki.
http://sportpesa.co.tz/adults_only
http://www.gamingboard.go.tz/