Twenzetu Duniani Na SportPesa 100Mil - Vigezo Na Masharti
Utangulizi wa Promosheni
SportPesa Tanzania inayofuraha kutambulisha Promosheni ya Twenzetu Duniani na SportPesa, kampeni maalum ya promosheni itakayofanyika katika kipindi cha mashindano ya Kombe la Dunia 2026. Promosheni hii inawapa wateja watakaokidhi vigezo fursa za kushinda zawadi za fedha kila wiki na kufuzu kushiriki Droo Kuu kwa kuweka dau zinazokidhi vigezo kupitia majukwaa ya SportPesa katika kipindi cha promosheni. Kushiriki promosheni hii kunamaanisha kukubali Vigezo na Masharti haya.
Dau zote zinazokidhi vigezo zitakazowekwa kuanzia tarehe 16 Juni 2026 hadi 19 Julai 2026 Saa 5:59 usiku kwa saa za Afrika Mashariki (EAT) zitastahili kushiriki katika promosheni hii. Wateja wataingizwa moja kwa moja kwenye promosheni watapoweka dau zinazokidhi vigezo katika kipindi cha promosheni. Hakutakuwa na usajili wa ziada unaohitajika. Kila dau linalokidhi vigezo litampa mteja nafasi moja ya kushiriki katika droo za promosheni.
SUKA MKEKA WAKO HAPA AU CHEZA KASINO
Vigezo Vya Kushiriki
Promosheni hii iko wazi kwa:
a. Wateja waliosajiliwa wa SportPesa Tanzania.
b. Wateja wenye umri wa miaka 18 na kuendelea.
c. Wateja watakaoweka dau zinazokidhi vigezo katika kipindi cha promosheni.
Wafuatao hawataruhusiwa kushiriki:
- Watu wenye umri chini ya miaka 18.
- Wafanyakazi wa SportPesa Tanzania na kampuni zake shirikishi.
- Wanafamilia wa karibu wa wafanyakazi wa SportPesa.
- Mtu yeyote ambaye haruhusiwi kisheria kushiriki katika shughuli za kubashiri au michezo ya kubahatisha.
Dau Zinazokidhi Vigezo
1. Aina zifuatazo za dau zinastahili kushiriki katika promosheni:
- Single Bets (Dau za Mechi moja)
- Multi Bets (Dau za Mechi zaidi ya moja)
- Live Bets (Dau za Mechi zinazoendelea)
- Mid-week Jackpot
- Supa Jackpot
- Michezo yote ya Casino inayopatikana kwenye majukwaa ya SportPesa Tanzania katika kipindi cha promosheni..
- Dau hairishwa (Cancelled) au zilizobatilishwa (Voided) hazitastahili kushiriki kwenye promosheni.
- Hakuna kima cha juu cha idadi ya nafasi ambazo mteja anaweza kupata kupitia dau zinazostahili..
Droo za Kila Wiki
Katika kipindi chote cha promosheni, SportPesa itaendesha droo za kila wiki
- Jumla ya washindi 100 watachaguliwa kila wiki.
- Tarehe za droo za kila wiki na mgawanyo wa zawadi vitatangazwa kupitia njia rasmi za mawasiliano za SportPesa.
- Washindi wa kila wiki watastahili kupokea mgao wa kiasi cha TZS 50,000,000 kwenye pochi zao, kwa mujibu wa ugawaji utakaoamuliwa na SportPesa Tanzania
- Wateja watakaoshinda zawadi za kila wiki wataendelea kustahili kushiriki katika Droo Kuu. Hivyo, mteja anaweza kushinda zaidi ya zawadi moja katika kipindi cha promosheni.
Droo Kuu ya Fainale
Droo Kuu ya Fainale itafanyika tarehe 20 Julai 2026.
- Wateja wote walioweka dau zinazostahili katika kipindi chote cha promosheni watastahili kushiriki katika Droo Kuu.
- Jumla ya washindi 10 watachaguliwa kutoka miongoni mwa washiriki wote waliokidhi vigezo katika kipindi cha promosheni.
- Zawadi ya Droo Kuu ya TZS 50,000,000 itagawanywa kwa usawa kati ya washindi hao 10.
- Washindi watataarifiwa na SportPesa Tanzania kabla ya hafla ya kukabidhi zawadi (ili kurahisisha mipango ya usafiri kwa washindi watakaotoka mikoani, yani nje ya Dar es Salaam).
Uchaguzi wa Washindi
- Washindi watachaguliwa kupitia mfumo wa kompyuta wa droo za bahati nasibu utakaosimamiwa na SportPesa Tanzania.
- SportPesa ina haki ya kuteua wakaguzi huru, wadhibiti au wawakilishi wa upande wa tatu kusimamia mchakato wa droo pale inapohitajika..
- Matokeo yote ya droo yatakuwa ya maamuzi ya mwisho.
Taarifa Kwa Washindi
- Washindi wa kila wiki watataarifiwa kupitia ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) na taarifa za simu zitakazotumwa kwenye namba iliyosajiliwa kwenye akaunti yao ya SportPesa.
- Washindi wa Droo Kuu watataarifiwa kwa simu kutoka Kitengo cha Huduma kwa Wateja kwa kutumia namba iliyosajiliwa kwenye akaunti yao ya SportPesa.
- Endapo mshindi wa Droo Kuu hatopatikana baada ya jitihada za kuridhisha kufanyika, SportPesa itakuwa na haki ya kuchagua mshindi mwingine.
- Ni wajibu wa Wateja kuhakikisha taarifa za akaunti zao ni sahihi na za sasa.
Malipo ya Zawadi Za Promosheni
- Zawadi zote zitawekwa au kulipwa kupitia njia itakayoamuliwa na SportPesa Tanzania.
- SportPesa ina haki ya kuthibitisha utambulisho wa mshindi kabla ya kulipa zawadi.
- Kushindwa kutoa nyaraka za uthibitisho zinazokubalika kunaweza kusababisha mshindi kupoteza haki ya kupata zawadi.
Matangazo na Uhamasishaji
Kwa kushiriki katika Droo Kuu, washindi wanakubali kwamba SportPesa Tanzania inaweza kutumia majina yao, picha, sauti ziliyorekodiwa, video ziliyorekodiwa na ushuhuda wao kwaajili ya matangazo, mauzo na uhamasishaji bila fidia yoyote ya ziada.
Kucheza kwa Kuwajibika
- Kubashiri kunaruhusiwa kwa watu wenye umri wa miaka 18 na kuendelea tu.
- SportPesa Tanzania inahamasisha kucheza kwa kuwajibika wakati wote.
- 12.3. Wateja wanashauriwa kucheza kwa kuwajibika na ndani ya uwezo wao wa kifedha.
Ubashiri unapaswa kuwa burudani. Ikiwa unahisi kuwa ubashiri wako unakuwa tatizo, tafadhali tembelea sportpesa.co.tz/responsible-gaming au wasiliana na timu yetu ya Huduma kwa Wateja inayopatikana saa 24 kwa siku, siku 7 za wiki.
Masharti Ya Jumla
SportPesa Tanzania inahifadhi haki ya kuchukua hatua yoyote kati ya zifuatazo, kwa kuzingatia idhini ya awali ya Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania:
a. Kurekebisha Vigezo na Masharti haya wakati wowote.
b. Kusimamisha, kubadilisha au Kusitisha promosheni hii pale inapohitajika.
c. Kumwondoa mshiriki yeyote anayeshukiwa kufanya udanganyifu, matumizi mabaya, kuathiri mchakato wa promosheni au kukiuka Vigezo na Masharti haya.
d. Kufanya maamuzi yote ya mwisho yanayohusiana na promosheni.
Endapo kutatokea mgogoro unaotokana na au unaohusiana na Promosheni hii, mgogoro huo utatatuliwa kwa mujibu wa sheria husika za michezo ya kubahatisha zinazotumika
Kukubali Masharti
- Kushiriki katika Promosheni ya Twenzetu Duniani na SportPesa kunamaanisha kukubali kikamilifu Vigezo na Masharti haya.
- Vigezo na Masharti yalioainishwa humu yatasomwa pamoja na Vigezo na Masharti ya Jumla ya SportPesa Tanzania, yanayopatikana kwenye tovuti ya kampuni. Kwa masuala yoyote ambayo hayajaelezwa wazi katika hati hii, Vigezo na Masharti ya Jumla yatatumika. Endapo kutakuwa na mgongano au kutokuwiana kati ya nyaraka hizi mbili, Vigezo na Masharti haya ya Promosheni yatakuwa na nguvu ya kutumika katika promosheni hii.
http://sportpesa.co.tz/adults_only
http://www.gamingboard.go.tz/